Tuesday, December 30, 2008

Chadema Out Of Competition!


Fighting for political powers in My home Constituency!


http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=8905
Date::12/29/2008
Chadema yaenguliwa uchaguzi Mbeya vijijini
Na Brandy Nelson na Peter Edson
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeenguliwa kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Mbeya Vijijini baada ya mgombea wake, Sabwee Shitambala kuondolewa katika orodha ya wagombea kutokana na Tume ya Uchaguzi kukubali pingamizi dhidi yake lililowekwa na vyama viwili.
Kwa mujibu wa barua iliyotolewa na kusainiwa na mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi jimboni hapo, Juliana Malange mgombea huyo wa Chadema hataruhusiwa kushiriki kwenye uchaguzi huo ulioandaliwa kuziba pengo lililoachwa na Mbunge Richard Nyaulawa aliyefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.
"Kutokana na pingamizi lililowekwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF) maombi yao yamezingatiwa na hivyo mgombea wa Chadema hataweza kuendelea na kampeni zozote za uchaguzi," inaeleza sehemu ya barua hiyo.
Uongozi wa Chadema mkoani Mbeya ulithibitisha kupokea barua yenye maamuzi hayo na kusema kuwa wanatarajia kukaa kikao baadaye jana usiku ili kujua hatima ya chama chao.
Mamia ya mashabiki wa Chadema waliokuwa wamejikusanya katika ofisi za msimamizi wa uchaguzi walionekana kujikusanya katika makundi baada ya uamuzi huo kutolewa, wengi wakiilaani hatua hiyo ya tume ya uchaguzi.
Katibu mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa alisema amesikitishwa na uamuzi huo kwa kuwa umekifanya chama hicho pamoja na wadau wengine kupoteza imani na usimamizi unaoendelea katika mchakato wa kumpata mbunge atakayerithi kiti cha Marehemu Nyaulawa.
Alisema tayari wameshapata taarifa za pingamizi dhidi ya mgombea wao kwamba limetupiliwa mbali na lile la CUF na CCM kukubalika jambo ambalo alisema limezua utata ndani ya chama chake.
"Tunajiandaa kukata rufaa ndani ya masaa 48 yajayo ili tuweze kupata haki yetu ya msingi dhidi ya mgombea wetu ambaye tunaamini kuwa alikuwa na vigezo vyote vtya kushiriki kwenye uchaguzi," alisema Dk. Slaa.
"Mimi sipo Mbeya ila tumepewa taarifa kuwa ombi letu limetupiliwa mbali, wenzetu wa CCM na CUF wamekubaliwa... jambo hili limetufanya tupoteze imani," aliongeza.
Taarifa dhidi ya pingamizi ya mgombea wa chama hicho ziliwakilishwa kwa msimamizi huyo wa uchaguzi jimboni hapo zikieleza kuwa Shitambala alikwenda kuapa katika kampuni ya uwakili badala ya mahakama ya wilaya, kitendo ambacho kimeelezwa kuwa ni kinyume cha sheria.
Juzi Shitambala aliwekewa pingamizi na vyama vya CUF na CCM. Chadema ilimwekea pingamizi mgombea wa CCM kwa madai kuwa alisema uongo kuhusu mahali alipozaliwa.
Vuta nikuvute hiyo ilitokea katika ofisi ya msimamizi wa uchaguzi huo ambako CUF na CCM walidai kuwa mgombea wa Chadema aliapa kinyume na taratibu za uchaguzi.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwasilisha fomu ya pingamizi hilo, mjumbe wa tume ya uchaguzi ya CUF, Hussein Mmasi alisema chama chake kiliamua kumwekea pingamizi Shitambala kutokana na kuapa katika kampuni ya uwakili badala ya Mahakama ya Wilaya.
Madai hayo ndio pia yaliyoifanya CCM kumwekea pingamizi mgombea huyo.
Wakati huohuo, CUF imesema kuwa kinazitambua mbinu zinazotumiwa na CCM katika kuhakikisha kinapata ushindi kwa kuvuruga daftari la wapiga kura na kuongeza idadi watu kwa miujiza, ikidai kuwa hiyo ndiyo silaha yao kubwa.
Akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kuzindua kampeni uchaguzi wa ubunge Mbeya Vijijini, naibu katibu mkuu wa CUF, Duni Haji alisema kuwa chama chao kinahitaji mabadiliko na kimekuwa na nafasi kubwa ya kushinda katika chaguzi mbalimbali, lakini tatizo kubwa ni mbinu chafu zinazotumiwa na CCM.
Duni alisema kuwa CCM huvuruga daftari na kuongeza idadi ya wapiga kura kimiujiza na mwisho wake huwa ni matokeo ya kura kuonyeha idadi kubwa tofauti na idadi ya waliojiandikisha.
Naibu katibu huyo alifafanua kuwa mbinu nyingine ni ile ya kumwaga polisi vijijini ili kuwajengea hofu wananchi.
"Mbinu zote hizo zinazotumiwa na CCM zina lengo la kuwaibia kura wapinzani huku wakijua mshindi anapotangazwa, wapinzani huenda mahakamani, lakini hurudi mikono mitupu kwa kuwa wao ndio serikali," alisema.
Alisema kuwa pamoja na CCM kutumia mbinu hizo chafu, bado CUF haitakata tama kudai haki na kuendelea kuwaelimisha wananchi juu ya kuacha tabia ya kuuza shahada zao.

I can See Some You Now!

It is long time since I once saw some of you,I can now see you and some of you don't even know how I can see you.This is what we call Technology,It can just take seconds for me to get to see you pictures!
I can see those faces,I really miss you all an I wish you all A happy New Year!
But I don't know that very small kid!Everything has changed,Soon I will go to see all those changes.























































Monday, December 29, 2008

My Grandfather Is Growing Older!




















My lovely grandfather is growing Old and as he grows Old the house also grow old.I can see how lonely the grandparents are after all the other family members are away to other cities and countries.
I really thank you grandfather cause without you I don't know how I could have been today.I know you made me stronger and you fought for me in whatever Situation and may God bless you and give you a longer life.I will try to pay you back by doing something to the family and all those in need of my Help.I know there is nothing to pay back to you but just say thank you!
I will see you soon!
His name is Samwel A.Swila,He is one of the wonderful grandfather i have seen,He was ready to fight for me at whatever cost.Even if fighting for me was at the expense of his happiness he always fought.Whoever has lived with me It is all his work with the Help of his almighty.

Mchakato Wa Uchaguzu Mbeya Vijijini


Chadema Vs CCM in my Home!

http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=8873

Date::12/28/2008
Mgombea wa Chadema awekewa pingamizi
Brandy Nelson, Mbeya
MCHAKATO wa uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Mbeya Vijijini umeingia dosari baada ya mgombea wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)Sabwee Shitambala kuwekewa pingamizi na vyama vya CUF na CCM.
Wakati mgombea huyo wa Chadema akiwekewa pingamizi, Chadema imeeleza kumwekea pia pingamizi mgombea wa CCM kwa madai kuwa amesema uongo kuhusu mahala alipozaliwa.
Vuta nikuvute hiyo ilitokea jana katika ofisi ya msimamizi wa uchaguzi huo ambako CUF na CCM wamedai kuwa mgombea wa Chadema ameapa kinyume na taratibu za uchaguzi.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwasilisha fomu ya pingamizi hilo mjumbe wa tume ya uchaguzi ya CUF, Hussein Mmasi alisema chama chake kimeamua kumuwekea pingamizi mgombea wa Chadema kutokana na kuapa katika kampuni ya uwakili badala ya mahakama ya wilaya.
"Tumeweka pingamizi kutokana na mgombea wa Chadema kuapa katika kampuni ya uwakili ambako yeye anafanyia kazi. Kufanya hivyo ni sawa na mgombea huyo kujiapisha mwenyewe,"alisema.
Alisema taratibu za kisheria zinawataka wagombea kuapa mahakamani na siyo kwenye makampuni ya uwakili, kwani fomu ya mgombea wa Chadema inaonyesha mhuri wa kampuni ya mawakili ambayo ndiyo anayofanyia kazi.
Madai hayo ndio pia yaliyokifanya Chama Cha Mapindizi kumwekea pingamizi mgombea huyo.
Akizungumza na gazeti hili, Mkurugenzi wa vijana wa Chadema John Mnyika, alikiri kuwepo pingamizi hilo na kueleza kuwa chama kimejipanga kulipangua.
Alisema viapo vilikuwa wazi na Chadema imejipanga kuliondoa pingamizi hilo.
Akizungumzia suala la pingamizi la mgombea wake, Mnyika alisema limewekwa kimakosa kwani mawakili ambao ni makamishna wa uchaguzi wa wilaya wanaruhusiwa pia kuwaapisha wagombea.
Alisema mgombea wa Chadema alilazimika kuapishwa na wakili kutokana na mahakama kufungwa siku za sikukuu.
Katika hatua nyingine Chadema kimemwekea pingamizi mgombea wa CCM Mchungaji Luckson Mwanjali kwa madai kuwa mgombea huyo alitoa taarifa za uongo kuhusu mahali alipozaliwa.
Akizungumzia pingamizi hilo mjumbe wa kamati kuu ya Chadema na ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Mpanda Kati, Said Arfi alisema wameamua kutoa pingamizi hilo kutokana na mgombea huyo kutoa taarifa ya uongo kuwa ni mzaliwa wa Igawilo kitongoji cha Uyole jijini Mbeya huku taarifa zinaonyesha kuwa ni mzaliwa wa Tukuyu wilayani Rungwe.
"Tumeamua kuweka pingamizi dhidi ya mgombea wa CCM kutokana na kuwepo kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoa sababu za uongo za mahali alipozaliwa na tumemtaka mgombea huyo awasilishe vielelezo vitakavyothibitisha sehemu halali aliyozaliwa,"alisema.
Alizitaja sababu nyingine za pingamizi hilo kuwa ni Mgombea huyo kutotoa tamko
la kisheria kuhusu maslahi yake katika hospitali teule ya Wilaya ya Mbeya ya Ifisi
na kwamba siye mgombea aliyethibitishwa na chama chake cha CCM.

Sunday, December 28, 2008

Ubunge Mbeya Vijijini


http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=8868
Mambo ya Harakati za Ubunge Mbeya Vijijini.
Urejeshaji fomu wafunika Mbeya Vijijini
Na Brandy Nelson, Mbeya
SHAMRASHAMRA na chereko jana ziliifunika Ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Mbeya vijijini kutokana na mashabiki wa vyama kuwasikidikiza wagombea wao kurejesha fomu kwa maandamano.
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ndio waliokuwa wa kwanza kurejesha fomu huku mgombea wao Sambwee Shitambala akisindikizwa na mamia ya wafuasi wa chama hicho waliokuwa wakiimba nyingi za kejeli dhidi ya Chama cha Mapinduzi.
Huku wengine wakiimba, CCM fisadi, CCM fisadi, wengine walikuwa wamebeba bendera za chama hicho wakiwa na magari, baskeli na pikipiki.
Katika ofisi hizo wafuasi wa Chadema kutoka katika
maeneo mbalimbali ya Mbeya Vijijini waliotembea kwa mguu kutoka katika ofisi za chama hicho zilizoko maeneo ya Mama John kwa maandamano, walijazana wakishuhudia mgombea wao akirejesha fomu.
Kwa upande wake CCM, walianza maadamano yao Mbeya Vijijini mapema asubuhi wakiwa na magari yaliyojaa wapambe huku mgombea wao, Lackson Mwanjali akiwa juu ya gari akipungia mkono watu waliokuwa pembeni ya barabara.
Hata hivyo, msafara wake ulipata msukosuko alipofika katika eneo la Stendi na Soko la Mbalizi Mbeya vijijini alipokutana na watu waliomzomea.
Katika hali isiyo ya kawaida wananchi na waliokuwa pembezoni mwa barabara walionekana ni wafuasi wa vyama vingine waliuzomea msafara huo huku wakipiga kelele za mafisadi , mafisadi na kusababisha mgombea huyo kukerwa na hali hiyo.
Baada ya kuonekana makelele yanazidi aliamua kuwapa ishara kwa kunyosha vidole viwili juu vya mkono wa kushoto na kimoja cha mkono wa kulia kupachika katikati ya vidole hivyo.
Hali hiyo ilisababisha mji mdogo wa Mbalizi kuzidi kwa makelele na kumzomea, hali ambayo iliulazimu msafara wake kusitisha maadamano na kurejesha fomu kimya kimya.
Akizungumza baada ya kurudisha fomu zilizopokelewa na Msimamizi wa Uchaguzi, Juliana Malange, mgombea wa Chadema, Sambwee Shitambala alisema ameamua kugombea uongozi katika jimbo hilo ili kudhihirisha kuwa wananchi wa jimbo hilo wanataka maendeleo.
Shitambala alisema wakati wa mabadiliko umefika sasa na kuwaahidi wananchi wa jimbo hilo kuwa hajagombea ili awe mtawala bali amekuja kuwatumikia wananchi wa jimbo hilo waliozingirwa na umasikini tangu nchi hii ilipopata uhuru miaka 45 iliyopita.
Wengine waliorudisha fomu ni pamoja Subi Mwakapiki wa Chama cha Sauti ya Umma na Daud Mponzi wa Chama cha wananachi (CUF).
Kampeni za uchaguzi huo wa kuziba nafasi iliyoachwa kufuatia kifo cha mbunge wa jimbo hilo, Richard Nyaulawa, zinatarajiwa kuanza Desemba 30 mwaka huu.
Wakati huo huo, Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM Mkoa wa Mbeya, Godfrey Mwamboma amekihama chama hicho na kujiunga na Chadema.
Mwamboma ni miongoni mwa wananchi wengine 102 wa vijiji vya Itewe, Inyala na Idunda vilivyopo katika kata ya Inyala Wilaya ya Mbeya vijijini waliorudisha kadi za CCM na kujiunga na Chadema huku wadai kuhama kwa sababu chama hicho kimewatelekeza tangu walipokichagua mwaka 2005.
Mwamboma aliyekuwa na kadi ya CCM namba 177601 iliyotolewa Julai 22 mwaka 2003, alichukua kadi ya Chadema yenye namba 0139981 ambayo alikabidhiwa na mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Said Arfi.
Alisema kuwa kuwa ameamua kwa hiari yake kujiunga na Chadema kutokana kuonesha muelekeo wa maendeleo wenye nia ya kulikomboa jimbo hilo na kuleta maendeleo ya kiuchumi.
"Kama kijana nilikuwa na matumaini kwamba CCM itawavusha na kuwakwamua kiuchumi lakini matokeo yake viongozi wakuu wa serikali wameonekana wazi wakituhumiwa kwa ufisadi na ulaji wa rushwa, jambo ambalo limenifanya nikose
imani na chama hicho," alisema
Wanachama hao walisema kuwa viongozi wa CCM walifika hapo wa kampeni za uchaguzi mwaka 2005 na kuwagawia nguo, kofia na kanga na baada ya hapo hawajarudi tena kijijini
hapo.
"Kitendo kilichofanywa na viongozi wa CCM kimesababisha tukione chama hicho hakina nia ya kutekeleza ahadi walizotuahidi wakati wa kampeni, hivyo tumeamua kukiacha na kujiunga na Chadema na ndiyo mkombozi wetu," alisema.

Monday, December 22, 2008

CCM yampiga chini Makamba-Harakati za Mbeya kupata MP



CCM yampiga chini Makamba
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimemteua mgombea wake wa ubunge jimbo la Mbeya Vijijini na kumwengua katibu wake mkuu, Yusuf Makamba katika safu za mbele za kutetea ushindi katika uchaguzi huo.CCM inafanya mikakati mizito ya kuhakikisha hakianguki kwa mara ya pili mfululizo baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kupata ushindi mkubwa kwenye uchaguzi mdogo wa jimbo la Tarime, ambako CCM iliongozwa na Yusuf Makamba.Kuanguka kwa CCM kulisababisha lawama kubwa dhidi ya Makamba kiasi cha kubashiriwa kuwa mkuu huyo wa zamani wa mkoa wa Dar es salaam angevuliwa ukatibu mkuu wa chama wakati wa mkutano wa Halmashauri Kuu uliofanyika Dodoma karibu mwezi mmoja uliopita.Makamba aliokoka baada ya kikao hicho kuisha bila ya kumjadili, lakini sasa hataongoza kampeni ya kutetea kiti kilichoachwa wazi na Richard Nyaulawa aliyefariki dunia kutokana na kuugua kwa muda mrefu.Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chiligati aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa Makamba sasa hatakuwa msimamizi mkuu bali mwangalizi na mwezeshaji wa kampeni."Makamba sasa hatajikita moja kwa moja katika usimamizi wa kampeni hizo kama ilivyokuwa Tarime badala yake atakuwa na kazi ya kuangalia na kuwezesha kampeni hizo," alisema Chiligati.Alisema uamuzi wa kutomuweka Makamba kuwa msimamizi mkuu unatokana na mkakati wa chama hicho kuiachia CCM Mkoa kufanya kazi hiyo, badala ya kuongozwa na CCM Taifa."Makamba atakuwa akienda Mbeya kuwezesha kampeni hizo na kurudi," alisema Chiligati. "Kamati ya uchaguzi ya mkoa wa Mbeya ndiyo yenye jukumu la kusimamia uchaguzi huo."Katika uchaguzi wa jimbo la Tarime, Makamba alilaumiwa kuwa hakufanya jitihada za kuondoa tofauti za makundi yaliyoibuka wakati wa uchaguzi wa mwaka 2005, moja likidaiwa kuongozwa na Kisyeri Chambiri na jingine likidaiwa kuongozwa na Chrisopher Gachuma.Makamba anadaiwa kuegemea kwenye moja ya makundi hayo na hivyo kuwafanya baadhi ya Wana-CCM kutomuunga mkono mgombea wake, Christopher Kangoye.Makamba pia alidaiwa kutotumia wazawa wa Tarime kwenye kampeni hizo na badala yake kuwatumia wapiga debe waliojiunga na CCM kutoka vyama vya upinzani, huku lawama nyingine zikielekezwa kwa kada huyo kwa kushindwa kwenye uchaguzi licha ya kuwezeshwa kila kitu, zikiwemo helkopta mbili.Kuhusu mgombea wa CCM kwenye jimbo hilo la Mbeya Vijijini, Kapteni Chiligati alimtangaza Mchungaji Luckson Mwanjale kuwa ndiye aliyeshinda katika uteuzi huo uliofanywa na Kamati Kuu ya CCM (CC) jijini Dar es Salaam jana.Alisema Mwanjale amewashinda wenzake kadhaa, akiwemo aliyekuwa mkuu wa majeshi mstaafu, Robert Mboma aliyepata kura 164.Wengine walioshiriki katika nafasi ya kugombea kuteuliwa ni Allan Mwaigaga, aliyepata kura 259, Adrea Sayile (229), Diovita Diame (162), Petro Mwashusha (28),Flora Mwalyambi(26), Machael Mponzi (23) na Maria Mwambanga(19).Alisema kampeni za uchaguzi huo wa Mbeya Vijijini zitazinduliwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi Januari 4 mwakani.Uchaguzi mdogo jimbo la Mbeya Vijijini utafanyika Januari 25 mwakani kuziba pengo la aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Richard Nyaulawa aliyefariki dunia Novemba mwaka huu kwa ugonjwa wa saratani.Wakati CCM imemteua mgombea wake, Chadema ilimteua Sabwee Shitambala kukiwakilisha katika uchaguzi huo utakaohusisha pia Chama cha Wananchi (CUF). Mgombea wa CUF anateuliwa leo kwenye mkutano mkuu wa CUF wilayani Mbeya Vijijini
window.google_render_ad();

Sunday, December 21, 2008

Shida Za Watanzania Zitaisha lini?


Watanzania Wanahitaji kudai Uhuru Wao.
Nadhani Tanzania iko chini ya Advanced Neocolonialsim ambapo uchumi umeshikwa na watu wa nje, wakati serikali imeshikwa na watanzania wasiokuwa na mapenzi na nchi hii na tayari ama wana maskani yao nje ya nchi au wana mipango ya namna hiyo.Kwa nini?(a) Aliyekuwa Gavana wa Benki kuu akisimamia wizi mkubwa wa pesa zetu, baada ya kuacha ofisi alirudi kwake Marekani, ambako ndiko alikomalizia maisha yake. (b) Aliyekuwa mwanasheria mkuu wa serikali akisimamia mikataba mingi mibovu, amegundulika kuwa na vijisenti vingi sana huko kwenye mabenki ya nje. Siku yoyote akitaka ataondoka na kwenda kwenye vijisenti vyake. Huyu bwana naye alikuwa ametushikia bendera ya karatasi tu. (c) Aliyekuwa katibu Mkuu wa wizara ya fedha akisimamia matumizi na mapato ya serikali yetu ana maskani yake ya kudumu huko Marekani. Siku yoyote anaweza kuondoka.(d) Leo hii nimesoma headline moja kuwa aliyekuwa waziri wa elimu akisimamia kuharibika kwa elimu nchini ili vizazi vijavyo viweze kutawaliwa kirahisi naye ana mpango wa kuhamie Marekani.(e) Kuna tetesi kuwa kiongozi mmoja mzito sana anauza mali zake kwa kasi sana, inawezekana lengo lake ni kuhamia nje ya nchi kutokana na mwenendo wa kesi za ufisadi zilizoanza. Kiongozi huyu anasemekana ana majumba Marekani na Afrika ya Kusini.(f) Viongozi wetu wengi waliowahi kushika nafasi nyeti wana maskani mengine nje ya nchi wakati hakuna viongozi wa nchi za nje walio na maskani yao nchini mwetu.Huu ufisadi tunaosikia kila siku ni matokeo ya viongozi wetu kuitumia nchi yetu kama sehemu ya wao kuchuma, halafu wakalie walichochuma huko nchi za nje. kwa kifupi, tunahitaji uhuru wetu tena, safari hii ikiwa ni dhidi ya Advaced Neocolonialism.

Thursday, December 18, 2008

Wakili ashinda kura za maoni Chadema Mbeya Vijijini


2008-12-18 12:33:47 Na Thobias Mwanakatwe, Mbeya
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimekamilisha mchakato wa kushiriki katika uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Mbeya Vijijini unaotarajia kufanyika Januari 25, mwakani. Uchaguzi huo unafuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, marehemu Richard Said Nyaulawa, aliyefariki dunia mwezi uliopita kutokana na ugonjwa wa kansa ya ini. Jana, Mkutano wa Chadema wa Wilaya ya Mbeya Vijijini, ulimchagua wakili wa kujitegemea, Sambwee Shitambala, kuwania ubunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini kupitia chama hicho. Shitambala aliibuka mshindi katika mkutano wa kura za maoni uliofanyika katika Hoteli ya Tughimbe mjini Mbalizi kwa kupata kura 44 na kuwashinda washindani wake watatu. Wagombea walioangushwa katika kinyang`anyiro hicho ni Katibu wa Chadema Wilaya ya Mbeya Vijijini, Ipyana Seme aliyeambulia kura 18, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Nswila, Amos Nsote aliyepata kura 17 na mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Elimu (Duce), Burton Gwakisa, aliambulia kura saba. Kufuatia matokeo hayo, Shitambala, anasubiri kuidhinishwa na Kamati Kuu ya Chadema itakayokutana mjini Mbalizi ambapo viongozi wakuu wa chama hicho, Mwenyekiti wa Taifa, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Dk.Wilbroad Slaa watahudhuria. Akizungumza na Nipashe baada ya kutangazwa mshindi, Shitambala ambaye alipata Shahada ya Uzamili ya Sheria nchini Uingereza, alisema kwake siasa siyo ajira bali ni huduma kwa jamii. Alisema kama atachaguliwa na wananchi wa Jimbo la Mbeya Vijijini atahakikisha anatumia taaluma yake ya sheria kwa kuwasaidia kuwaelimisha wananchi elimu ya uraia ili wajue wajibu wao na kuzifahamu haki zao za msingi. Alisema zipo baadhi ya sheria ambazo bado ni kandamizi kwa jamii hivyo atakapoingia bungeni atasaidia kuzipigia kelele ili zirekebishwe. Wakati huo huo, wanachama wawili wa Chama cha Wananchi (CUF) wamejitokeza kuchukua fomu, akiwemo Askofu wa Kanisa la Pentekoste, ili kugombea ubunge wa jimbo hilo. Katibu wa CUF Mbeya Vijijini, Ernest Gunza, akizungumza na Nipashe alisema miongoni mwa wanachama waliochukua fomu za kuwania ubunge ni Askofu wa Kanisa la Pentekoste PCG Mbeya, Samson Mwalyego, na mfanyabiashara wa mji wa Mbalizi, Obadia Nkyenky. Alisema zoezi la kuchukua fomu bado linaendelea hadi kesho. Katika hatua nyingine, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, ZittoKabwe, amesema chama chake hakipingi ushirikiano wa vyama vya upinzani katika kumweka mgombea mmoja kwenye uchaguzi wa Jimbo la Mbeya Vijijini.

Wednesday, December 17, 2008

After four Years Of Not Seeing you!

Today I was able to see Mwite and My mum again atleast by pictures after the three years of not seeing each other.This was possible only after giving Mwite my Laptop and Camera and by using the office internet of where she is doing her field training.Even if I have not met them for all that time but now I can guess on how they are and may be can see how I can act accordingly.
As I can see my mum has turned black and little older,more white hairs coming!I know she misses me very much her only kid,and Her only hope in her future.The distance is a little problem but from today this will no longer be a problem.I will make sure I get her pictures update at given time intervals!Also soon I expect Mwite to show me the pictures of my lovely grandfather and all other people whom I have been missing for four years!
Thanks Mwite and God Bless you!







Mama Ninakukumbuka sana na wala sijakusahau!Ninakupenda sana!


Monday, December 15, 2008

Harakati za Uchaguzi Mbeya Vijijini!




Wapinzani sasa wasambaratika Mbeya Vijijini 2008-12-15 12:56:43 Na Joseph Mwendapole na Muhibu Said
Kambi ya upinzani, imeshindwa tena kuungana na kusimamisha mgombea mmoja katika uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Mbeya Vijijini. Uchaguzi huo umepangwa kufanyika Januari 25, mwakani. Jimbo hilo liko wazi kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wake, Richard Nyaulawa (CCM) kufariki dunia. Vyama vinne vya Chadema, NCCR-Mageuzi, TLP na CUF, vilianzisha ushirikiano ambapo vilikubaliana kuwa vitasimamisha mgombea mmoja katika chaguzi pale ambapo itaonekana chama kimojawapo kinaungwa mkono pamoja na kuwa na msimamo mmoja katika masuala mbalimbali ya kitaifa na kimataifa. Ushirikiano huo uliingia doa Oktoba, mwaka huu katika uchaguzi mdogo wa ubunge na udiwani katika kata ya Tarime Mjini na jimbo la Tarime wa kujaza nafasi hizo kufuatia kifo cha aliyekuwa anazishikilia, Chacha Zakayo Wangwe kufariki dunia. Katika uchaguzi huo, kambi ya upinzani ilishindwa kukubaliana kusimamisha mgombea mmoja hivyo Chadema, NCCR-Mageuzi kila kimoja zikasimamisha wagombea huku TLP ikikiunga mkono NCCR-Mageuzi na CUF kukiunga mkono Chadema. Democrat (DP) ambacho hakiko katika ushirikiano huo nacho kilisimamisha wagombea. Mwenyekiti wa DP, Christopher Mtikila, alisema jana kuwa chama chake kiko katika mchakato wa kumpata mgombea atakayesimamishwa kuwania jimbo hilo. Alisema wanatarajia mchakato huo utakamilika na hatimaye mgombea kupatikana wiki hii. Kwa upande wake, Chadema) kimesema kinatarajia kusimamisha mgombea na tayari mchakato umeanza. Katibu Mkuu wa Chama hicho, Dk. Willbroad Slaa, alisema uteuzi wa Wilaya utafanyika Desemba 17 na Kamati Kuu ya chama itakaa Desemba 20. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TLP, Augustino Mrema, alisema jana kuwa hajajua iwapo chama chake kitasimamisha mgombea au la. ``Nipe muda wa saa moja kisha nitakujibu kama tutasimamisha mgombea au la, ngoja niwasiliane na wenzangu ntakujulisha,`` alisema Mrema. Hata hivyo, gazeti hili lilipowasiliana naye baada ya muda huo Mrema hakupokea simu licha ya kupigiwa mara kwa mara. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Lipumba, alisema Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Shariff Hamad, ndiye atakayekuwa msimamizi wa mchakato mzima kwa upande wa kwa CUF katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Mbeya Vijijini. Alisema CUF kilimwandikia barua Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, ili chama hicho kikiunge mkono CUF katika uchaguzi huo lakini hadi jana Mbowe hakuwa ameijibu barua hiyo. Profesa Lipumba alisema CUF kitashiriki kikamilifu katika uchaguzi huo na wana matumaini ya kushinda kwa kuwa mgombea wao katika uchaguzi wa mwaka 2005 alishika nafasi ya pili nyuma ya marehemu Nyaulawa. Alisema ushirikiano wa kisiasa wa vyama vinne una mtihani mgumu kwa kuwa baadhi ya vyama vimeonyesha dalili zote za kudhoofika. Akizungumza na Nipashe jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NCCR-Mageuzi, Joseph Selasini, alisema wanasubiri uamuzi wa vikao vya juu vya chama hicho vitakavyoamua iwapo chama hicho kisimamishe mgombea au la. Alisema ingawa wana nia ya kumsimamisha mgombea wao, lakini kwanza watapima upepo kabla yakufikia uamuzi huo. Selasini alisema yeye alikuwa Mbeya kwa wiki tatu kufanya tathmini ya kisiasa na aliyoyaona huko yatawasilishwa kwenye vikao vya ngazi za juu ili yafanyiwe maamuzi. Mchakato wa uchaguzi huo mdogo umeashaanza rasmi baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kutoa ratiba yake inayoonyesha kuwa uteuzi wa wagombea utafanyika Desemba 27 wakati kampeni zitaanza rasmi Desemba 28 hadi Januari 24, siku moja kabla ya upigaji kura. Uamuzi wa kila chama kusimamisha mgombea wake unakipa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi nzuri ya kushinda kutokana na kambi ya upinzani kugawana kura.

Saturday, December 13, 2008

The Former Mkuu wa Majeshi(JWTZ) Struggling to Be our MP

http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?id=14560

Habari za Kitaifa
Habari zaidi!
Jenerali Mboma ajitosa kuwania kiti cha Mbeya Vijijini
Merali Chawe, MbeyaDaily News; Friday,December 12, 2008 @21:15
Habari nyingine
Wanafunzi vyuo vikuu waaswa kujaza fomu za kurejea darasani
Jenerali Mboma ajitosa kuwania kiti cha Mbeya Vijijini
Mkuu wa Majeshi mstaafu, Jenerali Robert Mboma jana alikuwa mwana-CCM wa tisa kuchukua fomu ya kuwania kuteuliwa kuwania nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Mbeya Vijijini na kumaliza uvumi uliokuwa umetawala kama atajitosa katika kinyang'anyiro hicho ama la. Kuingia kwa Jenerali Mboma katika kinyang'anyiro hicho ndani ya CCM kumebadili mwelekeo na kusababisha wanachama waliochukuwa fomu kuwania nafasi hiyo huku wakiwa na imani ya kuibuka na ushindi kuanza kupigana vijembe wao wenyewe. Akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kuchukua fomu, Mbona alipinga madai yanayotolewa na baadhi ya wanasiasa kuwa mstaafu huyo wa Jeshi ametumwa na Rais Jakaya Kikwete kuja kugombea katika jimbo hilo lililoachwa wazi na Richard Nyaulawa. "Mimi napiga vita sana kupigana vijembe, na hii ndio dalili yenyewe ya kupigana vijembe, Rais Kikwete kamwe hawezi kufanya kitu kama hicho," alisema na kuongeza kuwa ameamua kuingia katika kinyang'anyiro hicho kwa utashi wake mwenyewe. Aidha alisema ameamua kuingia katika ulingo wa siasa si kwa ajili ya kutafuta maslahi, lakini kwa sababu anataka kutatua kero zinazowakabili wananchi hususani suala la mbolea, umeme na maji, mambo ambayo yanakwamisha shughuli za kiuchumi za wananchi wa jimbo hilo. Alisema kuwa kabla ya siasa kutenganishwa na Jeshi alifanikiwa kushika nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya CCM na kwamba ana uzoefu na masuala ya siasa na kwamba ana imani akishinda ataweza kutatua kero mbalimbali za wananchi. Hadi kufikia jana mchana, wanaCCM tisa walikuwa wamechukua fomu za kuomba kuwania nafasi ya ubunge wa jimbo hilo, mbali ya Jenerali Mboma wengine ni Allan Mwaigaga, Djovita Diyami, Maiko Mponzi, Flora Mwalyambi, Petro Mwashusya, Mchungaji Luckson Mwanjali, Mariam Mwambanga na Andrew Sayila. Mwisho wa kuchukua fomu kwa wanaowania kuteuliwa na CCM ni leo saa 10 alasiri, ambapo kampeni za uchaguzi wa jimbo hilo zinatarajiwa kuanza Desemba 27 na uchaguzi unatarajia kufanyika Januari 25, mwakani. Wakati CCM leo ikikamilisha shughuli ya uchukuaji na urejeshaji fomu kwa wanachama wake, Chadema bado inaendelea na mchakato wa utoaji fomu utakaofikia tamati Desemba 15, ambapo kwa upande wa Chama cha Wananchi (CUF), tayari kimemtangaza Mwanamama Amina Ahmed kugombea katika jimbo hilo.


Friday, December 12, 2008

Mbeya Rural Constituency(My Home) Struggling to get New MP!




After The Death of the former MP in my place now people struggle to get new MP to cover the gap,Hope that this can be some efforts towards changing the life of the suffering Mbeya Rural
District residents!But this might be hard as the most of the people in the don't open their eyes
to see who can help them and also some even don't know that they got problems!
The kids in the picture above deserve a bright future,all this lies on the people who have the
dhamana including the MP's.It pains me a lot when i see at the end of the day all these kids
end up nowhere,They even don't how the other kids on the other world live.But one day I
believe more of those will have better opportunities!God help them!




Afisa Elimu wa Chunya achukua fomu kuwania jimbo la Nyaulawa 2008-12-12 13:01:23 Na Thobias Mwanakatwe, Mbeya
Afisa Elimu wa Wilaya ya Chunya mkoani hapa, Petro Mwashusa amekuwa mwanachama wa sita wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuchukua fomu za kuwania ubunge katika jimbo la Mbeya Vijijini. Katibu wa CCM Wilaya ya Mbeya Vijijini, Hassan Dumwali, alisema Afisa Elimu huyo ambaye ni mkazi wa Mbeya Vijijini, ni mwanachama pekee aliyechukua fomu jana kwani hadi kufikia saa 10:00 jioni ambao ndio muda wa mwisho kwa wanachama kuchukua fomu. Wanachama wengine waliokwishachukua fomu ni Djovita Diame ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Mbeya Vijijini, Mchungaji Langson Mwanjali (Katibu wa Fedha na Uchumi), Aran Mwaigaa (Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa). Wengine ni Flora Mwaliambi (Mjumbe wa Halmashauri (CCM Mbeya Vijijini) na Michael Mponzi ambaye ni mtoza ushuru kituo cha Igoma katika Halmashauri ya Mbeya Vijijini. Wakati wanachama wa CCM wakiendelea kuchukua fomu, kwa upande wa Chadema ndiyo kinaanza leo kutoa fomu kwa wanachama wake wanaotaka kuwania ubunge. Katika kuupa nguvu uchaguzi huo, tayari viongozi wandamizi wa Chadema toka makao makuu wameshawasili mjini Mbeya kupanga mikakati ya jinsi chama chao kitakavyoshiriki uchaguzi huo na kuibuka na ushindi. Viongozi hao bado hawajaanza mikutano ya hadhara na badala yake wanachokifanya kwa sasa ni kuitisha vikao vya ndani vya chama. Kwa upande wa Chama cha Wananchi (CUF) kimeanza kutoa fomu kwa wanachama wake wanaotaka kugombea ubunge ambapo hadi sasa Mwenyekiti wa Mbeya Vijijini wa chama hicho, Amina Ahmed ndiye mwanachama pekee aliyechukua fomu. Naye Kamishina wa NCCR Mageuzi, Adam Mwansampeta alisema chama chake kinaendelea na mikakati kwa ajili ya uchaguzi huo ingawa bado hakija weka wazi kama kitasimamisha mgombea wa ubunge wa jimbo hilo.

Thursday, December 4, 2008

RC Mbeya amtimua Mkurugenzi

RC Mbeya amtimua Mkurugenzi
na Christopher Nyenyembe, MbeyaMKUU wa Mkoa wa Mbeya, John Mwakipesile, katika hali iliyoonyesha kutoridhishwa na utendaji wa kazi wa Mkurugenzi wa jiji hilo, Elizabeth Munuo, amemwamuru aondoke kwenda kutafuta kazi nyingine kama kazi aliyonayo imemshinda.Mwakipesile alitoa kauli hiyo jana mara baada ya Munuo kulalama katika kikao cha bodi ya barabara kilichokutana mjini hapa kuwa anajuta na kujilaumu kuhamishiwa Jiji la Mbeya, lenye uchafu uliokithiri na lisilo na vitendea kazi.Munuo alitoa kauli hiyo alipotakiwa na wajumbe kuelezea mikakati ya kukabiliana na tatizo la uchafu katika jiji hilo, ambalo limekithiri kwa uchafu kila kona na kwenye lango kuu la kuingilia eneo la Uyole ambako kuna dampo kubwa la kutupia taka, lakini zinamwagwa taka hadi barabarani.Huku akisikilizwa kwa makini na wajumbe hao, mkurugenzi huyo badala ya kuelezea mikakati yake, alijikuta akiweka wazi uchungu alionao wa kujutia uamuzi wa serikali wa kumhamishia hapo, huku akidai kuwa mikoa aliyotoka haikuwa hivyo.“Hapa kwenu Mbeya, nilipokuja nilikuta hakuna wahisani, nasikia waliondoka baada ya kusumbuliwa na matukio ya ujambazi, nilikuta halmashauri ikiwa katika hali hiyo na tumeendelea hivyo hivyo na magari mawili ya kuzolea taka, bajeti ya mwaka huu tumeweka magari mawili ya taka angalau yatusaidie lakini jiji hili linahitaji magari 10,” alisema Munuo.Munuo alikiri kuwa jiji hilo limekithiri kwa uchafu ambao hauwezi kuondolewa kwa kutumia magari mawili, tena mabovu na kwamba ukosefu wa magari mapya umetokana na tatizo lililowaondoa wahisani.“Hata mimi mwenyewe najilaumu ilikuwaje nikahamishiwa katika mji huu waliofukuzwa wahisani na nimekuta hali chafu, miji yote niliyokaa ilikuwa na hali nzuri, si Mbeya ndugu mwenyekiti,” alisema mkurugenzi huyo.Ndipo Mkuu wa mkoa huo, Mwakipesile akionyesha wazi kuchukizwa na kauli ya mkurugenzi huyo ya kuubeza uamuzi wa serikali wa kumhamishia kwenye jiji hilo, aligonga meza na kumpasha kuwa kama ameshindwa kazi aondoke.“Kama huwezi kazi nenda, go goo, ondoka, katafute kazi sehemu nyingine, Where you think you can do a better job, go, go hatuwezi kufanya kazi kwa kubembelezana, go nenda, takataka zinatupwa hadi barabarani unatuletea utetezi hata mifereji mnashindwa kuzibua, no,” alisema Mwakipesile kwa ukali.Mbali ya mkuu wa mkoa huyo, kauli hiyo pia iliwafanya wajumbe wengine wa kikao hicho akiwemo Mbunge wa Viti Maalumu, Hilda Ngoye, ambaye alitahadharisha kuwa uchafu wa jiji hilo haupaswi kufumbiwa macho kwani unaweza kuwa chimbuko la matatizo mengi.Aliyefuatia alikuwa Mbunge wa Mbeya Mjini, Benson Mpesya, ambaye hakuridhishwa na hoja ya ukosefu wa vifaa vya usafi, isipokuwa alidai kuwa watendaji wa halmashauri hiyo hawajajipanga kukabiliana na tatizo hilo, hivyo kusababisha takataka zizagae kila kona.Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi, alisema inatia shaka kwa mtendaji wa serikali kudai kuwa kule alikokuwa, kulikuwa kusafi kuliko Jiji la Mbeya alikohamishiwa kwani hali hiyo inaonyesha upungufu wa uwajibikaji.“Hii ni changamoto kwako mkuu wa mkoa, kwa kuwa watu hawa unaishi nao kila siku na hali ya uchafu unaiona, ulichopaswa ni kutoa maagizo ya jiji liwe safi, unakumbuka Jiji la Dar es Salaam liliwahi kuvunjwa na kuwa mamlaka, sasa hatuoni sababu ya utetezi huu unaotolewa hapa wa kujutia kuhamishiwa Mbeya, ” alisema Zambi.Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, John Mwankenja, alimuomba, mkuu wa mkoa huo amtake mkurugenzi huyo afute kauli yake, kwa madai kuwa inadhalilisha utendaji mzima wa serikali katika jiji hilo.Mstahiki Meya wa jiji hilo, Athanas Kapunga, aliingilia kati kwa kukiri upungufu wa kuwapo kwa uchafu katika jiji leo.Alisema yote yaliyosemwa na wajumbe katika kikao hicho, yatazungumzwa na madiwani wa halmashauri hiyo, huku akielezea wazi kuwa mji huo umekuwa ukiendelea kushuka hadhi tofauti na miaka ya nyuma.Kwa upande wake Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, Zelothe Stephen, alilitaka jiji hilo kuhakikisha linaweka taa za barabarani kama urembo, lakini zitakuwa sehemu muhimu ya ulinzi kwa kupunguza vitendo vya uhalifu.“Mimi sitaki kujikita huko kwenye uchafu, mimi nahamia upande wa taa za barabarani, kwetu sisi taa ni ulinzi mkubwa, zinasaidia kupunguza upigaji wa nondo, hii inatia aibu badala ya Mbeya kuwa jiji, linakuwa zizi,” alisema Kamanda Stephen. Tanzania Daima

My Fantastic Diagnostic Class!

It is hard to believe but this happened today when I went to the Hospital For My Diagnostic Class,me with other five classmates one being my
friend from Yemen and the rest being my Chinese Classmates.For today our patient was someone who worked as the Head of Trainings for Moshi Police College during 1969-73.He didn't believe his eyes to see a Tanzanian Medical Student doing training in his ward,he called me 'rafiki'(friend-pengyou in Chinese) and also said a lot of other Swahili words,this was a big suprise to those classmates.This was a very big Advantage for the six of us cause we met someone who was ready to offer us with whatever information we needed for his sickness!Normally it is not easy here to get a patient who will be fully cooperative as the Doctors are enough and the patient is always in touch with his specialist.But this was a chance for me to make a lead on this as the patient has met a 'rafiki' who he has been looking for more than thirty years may be.Cause he lost contacts to all his old 'rafikis' of Moshi so today he can't believe to see a copy of them and seeing the product of the contribution he offered for Tanzania.Cause he said at that time the people he met most of them knew very little.
So it was like asking him the conditions of his disease while alternating with our Tanzanian Stories so that was so cool and even those five classmates had an opportunity to know something of Tanzania,something which is layer cause we never had a chance where we could talk about this.I asked which flight did he use when going to Tanzania,He laughed and said at that time they didn't take flight,They were going to Guangzhou and take a Boat/ship to Tanzania and that could take 15 days to arrive to Dar.But I told him that now he can just take flight from China and drop
at Kilimanjaro Airport ...he was so impressed!He just mention some Tanzanian fellow officials of
that college who were his friend like Hubert,Benkan,etc.He says if I have a way to see these guys I should pass greatings to them he misses them very much.
His wife or daughter called and he was very happy told her that today he had met a lost 'rafiki'... Also one Doctor came to our ward and was informed that the guy worked in Tanzania for 3 years and that Doctor made a guess that he went to Tanzania for TAZARA but he said no for that was a more advanced program than the TAZARA cause he was a big guy the head of Training at Moshi he had a chance to meet most of the big Government people he always mentioned of Karume.
He said when he comes out of Hospital we should arrange a meeting and he will invite me for
beer(the major cause of his Kisukari and which is the major reason why he is admitted) and I said Ok and took his Contacts and also gave my contacts.I'm sure this guy really want to see the products of his work of those years and he is not lack cause he stays out of the city where it is hard to meet any of his rafiki but the Hospital made him meet one and me I promise to continue to be a rafiki to him and I will try to get the contacts of his old rafiki so that one day they can even talk to each other.but I'm not sure of his Old Tanzanian rafiki if they are still there cause the guy is now 68 years old.
Anyway The Important thing is for us to make sure the people like these become proud with Tanzania due to their Contribution even if they can't see their old Tanzanian rafiki's they should see a shining country so that when they here news on TV or Newspapers they should talk to their friends that ,that country is of their old rafiki whom they cared for!
Dedication to all Old Chinese who did something for Tanzania in those years!





Tuesday, December 2, 2008

Sometimes It Is Like Home




Sometimes I feel like missing home too much, But at certain Situation like when visit some places around China and meet with other countrymates/Africans It is like I'm Home!Hope all those old friends who are in Iwindi,Mbalizi are all fine.
Most of my old friends, there is no way I can communicate to them now But I just want to let
their mind know that I really miss them and remember them with all the difficult times they face due to Country's bad rural situations.One day I will go there to see them and one day there lives if not their kids lives will change and be good!
In China also not everybody has good life,they also have Many people especially in the rural areas with bad life conditions but their country is trying to make sure conditions change to be better and atleast you can see them enjoying the good roads,schools,banks,water services,healthy services,supermarket etc.So to me there is a dream that Tanzania can also learn from China and we have all the potentials to make people enjoy their lives in Tanzania.
I miss Iwindi,Mbalizi,Mbeya,Tanzania and all thoese friends of mine whom we are no longer in touch!
To those who don't know Chinese when you meet Chinese just say:
'nihao'(habari-hi),
'pengyou'(rafiki-friend),
'huanying'(karibu-welcome),
'wo ai ni'(ninakupenda-I love you)
baba(baba-father)
mama(mama-mum)
gege(kaka-brother)
guojia(nchi-country)
If I see there is need I will deliver more Chinese Words next time!