Tuesday, January 6, 2009

Mboma: Kitambi kimeniangusha

mambo ya Home!
Mboma: Kitambi kimeniangusha
Hawa Mathias, Mbeya
ALIYEKUWA Mkuu wa Majeshi Nchini, Meja Jenerali, Robert Mboma, amesema anaamini kitambi alicho nacho kimesababisha kushindwa katika kura za maoni za Chama cha Mapinduzi (CCM) za ubunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini.
Mboma aliyasema hayo juzi wakati akiwashukuru wananchi katika uzinduzi wa kampeni za chama hicho za kinyang'anyiro cha ubunge wa jimbo hilo.
Alisisitiza kuwa anaamini kilichochangia kutopata kura nyingi zaidi ni kitambi
hicho alichokuwa nacho na kwamba hali hiyo itamkomaza kisiasa.
Mboma ambaye aliwashangaza baadhi ya watu walioshuhudia uzinduzi wa kampeni hizo uliofanywa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi katika kijiji cha Ilembo Mbeya vijijini.
alisema kkuanguka kwake katika jimbo hilo kumetokana
na wananchama wa chama hicho kumnyima kura.
Alisema kitendo hicho hakiotamuathiri bali wanamkomaza kisiasa na kwamba endapo kama angeteuliwa kuwa Mbunge wa jimbo hilo angelepeleka maendeleo.
"Kwa kweli nanawashukuru wananchi mlionipigia kura nilizozipata ingawa hazikuwa
ndogo lakini ninasikitika na ninawashukuru ambao hawakunipigia kura na kuniangusha wakati wakijua wazi kuwa mimi ni mzaliwa na hapa na mngenichagua ningewaletea wananchi maendeleo katika jimbo la Mbeya vijijini," alisema.
Aliendelea kusema kuwa sio mbaya hata kama wamemchagua Mchungaji Mwanjali kwa sababu anaimani atawaletea Maendeleo na kurithi yale yote aliyatarajia
kuyafanya aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo, Marehemu Richard Nyaulawa katika
kuboresha huduma za jamii hususan maji, umeme na kuboreshea miundombinu.
Kwa upande wake, Waziri wa Afya David Mwakyusa aliwatahadhalisha wapiga kura kuwa makini na Vyama vya Siasa hususan Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) a kwa kuzingatia sera zao na kwamba wawafananishe na Vyura wanaosubili kipindi cha Mvua na kuanza kukoroma katika mito.
Alisema vyama vya upinzani vinatakiwa kuangaliwa kwa umakini na kwamba kipindi hiki cha kampeni wanaanza kupita katika mikoa kuomba kura kwa wananchi na kutoa lugha chafu badala ya kujenga sera itakayoweza kukubalika kwa jamii na kwamba jamii inapaswa kutambua baadhi ya Vyama vya upizanzani havina ofisi za kuendeshea shughuli na kwamba watambue maendeleo hayaletwa kwa kasfa bali kwa sera ya chama husika.
"Kama kweli wananchi mtakuwa na mtazamo viongozi gani wanaoweza kuwaongoza wakiwa ni watu wa kwanza kukashfu nchi na chama je wakiwa madarakani watawaongoza vipi sasa mtambue msimu wa kampeni ndio wanapita kuomba kura wakati wa kampeni hamuwaoni je huu uongozi utatambua kero za wananchi na kuleta maendeleo"Alisema Mwakyusa.
Naye Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba, alisema kauli ya Chadema dhidi ya
Mwinyi, wameifananisha na mbio za sakafuni kutokana na dhamila ya ungozi wa chama hicho kumgeukia mwenyewe na kujitukana kutokana na mgombea wake kutolewa katika kinyanganyiro cha ugombea ubunge jimbo la Mbeya vijijini.
Makamba, alisema hakuna haja ya wananchi kukichagua chama cha Chadema na CUF kutokana na kuonyesha nidhamu yao na kwamba hawana uwezo wa kuleta maendeleo kutokana na kuonyesha wazi kashfa ya kumtukana kiongozi wa ngazi za juu ambaye aliwahi kuongoza nchi.
Akizindua kampeni hizo, Mwinyi alisema kuwa Vyama vya Siasa vilipaswa kupanua wigo kwa wananchi kwa kueleza sera za chama husika zitakazokubaliwa na wananchi na kuleta maendeleo .
Alisema vyama vya siasa vinapaswa kushindana katika Sera na si kushindana kwa
matusi, dharau na kejeli.
Alisema kutumia uungwana katika kampeni za uchaguzi vinaweza vikapata fursa ya
uongozi na kutatua matatizo ya wananchi kwa kutumia Sera za Chama husika.
Alisema kuwa vyama vilipaswa kila kinachofanywa kinafanywa kwa kufuata misingi na kanuni za katiba katika kugombea jimbo la Mbeya vijijini ili liwe na Amani Umoja
na Mshikamano na kujenga mzinga wa nyuki ulioshikimana katika kuleta maendeleo
Demokrasi,udugu, na muungano utakaolinda haki za wananchi na kuheshimu ,kuelimisha na kupata misingi bora katika jamii.
"Mimi nimekuja kuzindua kampeni na wala sijaja katika kupiga kampeni na kwamba
niliwashangaa sana viongozi wa chadema kwa kupanga kuja kutukana na matusi na kwamba hakuna chama kinachoendeshwa kwa kukejer na kutoa rugha chafu,"alisema mwinyi.

Saturday, January 3, 2009

CHADEMA Walizwa na NEC

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imetupilia mbali rufani ya mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Sambwee Shitambala, dhidi ya uamuzi wa Msimamizi wa Uchaguzi kumwondoa katika orodha ya wanaowania ubunge kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Mbeya Vijijini. Shitambala ambaye aliwasilisha rufani dhidi ya uamuzi wa Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Mbeya Vijijini, Desemba 30, mwaka jana baada ya kuwekewa pingamizi na wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF), kwamba alikiuka taratibu za ujazaji fomu hiyo, kwa kuapa kwa kutumia wakili badala ya mahakama kama sheria ya uchaguzi inavyoagiza. Akitolea uamuzi wa rafani hiyo Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Lewis Makame, alisema Tume ilimwita mrufani juzi kwa lengo la kupata maelezo ya ziada kuhusu sababu za rufani aliyowasilisha na kwamba, hayakupishana na yaliyoandikwa. Jaji Makame alisema kwa kuzingatia sababu za rufani, NEC iliona hoja tatu za msingi zilizokuwemo ambazo ni Je, tamko la kisheria lililotolewa na mrufani katika fomu zake za uteuzi ni halali kwa mujibu wa kifungu cha 38(3) (a) cha Sheria ya Uchaguzi Na. 1 ya mwaka 1985? Je, Sheria ya Viapo (The Oath and Statutory Declarations Act (CAP 34 R. E. 2002) na Sheria ya Wanaoidhinisha Viapo (The Notaries Public and Commissiners for Oaths Act (CAP 12 R.E. 2002) zinaweza kutumika katika suala hili? Alisema tatu,Tume iliangalia hoja ambayo wagombea walikuwa na muda wa kutosha wa kukamilisha fomu zao za uteuzi na kuziwasilisha kwa wakati? Aidha, Je,Tume inaweza kutumia ``proviso`` ya kifungu cha 38(4) cha Sheria ya Uchaguzi na. 1 ya mwaka 1985? Alifafanua kuwa baada ya kuzipitia hoja hizo za msingi, NEC ilibaini kuwa mgombea wa Chadema alikiuka taratibu ya kula kiapo kwa wakili aliyemtaja kwa jina la Evarist Martin Mashiba wa S L P 4185 Dar es Salaam na kugongwa muhuri wa wakili huyo na kwamba, kifungu cha 38(3) (a) cha Sheria ya Uchaguzi Na. 1 ya mwaka 1985 kimebainisha tamko linalotakiwa kufanywa na mgombea ubunge. ``Kila fomu ya mgombea uchaguzi lazima iambatane na tamko rasmi la kisheria ambalo limewekwa saini na mgombea mbele ya hakimu likitamka bayana sifa za mgombea na vile vile kutamka wazi kuwa mgombea hana pingamizi kugombea katika uchaguzi,`` alisema. Alisema hivyo katika kifungu hicho neno ``shall`` ndio lililotumika ambalo linaonyesha ni �lazima� mgombea kula kiapo mahakamani na kwa Hakimu Mkazi, Wilaya na Mahakama za Mwanzo hivyo ni dhahiri kwamba, wakili hapaswi kushuhudia tamko husika na tamko hilo litakuwa sio halali. Aliendelea kuwa kipengele cha Sheria za Viapo na Sheria ya Wanaoidhinisha Viapo, hakiwezi kutumika katika suala hilo kwa sababu Sheria ya Uchaguzi Na. 1 ya mwaka 1985 imetamka bayana kuhusu anayetakiwa kushuhudia tamko la kisheria la mgombea. Jaji Makame alisema NEC ilitangaza Desemba 17, wagombea kuchukua fomu na kurudisha Desemba 27, kwa maana hiyo kulikuwa na siku sita za kazi hivyo mahakama zilikuwa zinafanya kazi na wagombea walipaswa kutumia siku hizo kula kiapo kwa hakimu. Pia, Tume hiyo imeridhika na maelezo ya mrufani kuwa hakujiapisha mwenyewe na wala hajaajiriwa na Kampuni ya Evarist Mashiba Advocates kama ilivyodaiwa na mweka pingamizi. Kwa upande wa mgombea wa DP, naye amegonga mwamba rufani yake kama sababu za mgombea wa Chadema. Kwa upande wake, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema na Mbunge wa Mpanda Kati, Saidi Arfi, alisema chama kitakaa chini kutafakari uamuzi uliotolewa na Tume kwa sababu, ni pigo kwa demokrasia nchini. Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, alisema hivi sasa bado hawajaamua kuunga mkono CUF. ``Kwa kuwa jambo lenyewe limetokea sasa, tutakaa na kisha baadaye kutoa taarifa kamili kwa umma, kwa sasa bado tunatafakari,`` alisema Slaa. Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Januari 25, unafuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Vijijini, Richard Nyaulawa (CCM).

Friday, January 2, 2009

Mambo ya Mbeya Vijijini na Uchaguzi wa MP


Date::1/2/2009
Mambo magumu Mbeya Vijijini
*Hatima ya mgombea Chadema leo
Na Brandy Nelson, Mbeya
MAMBO yanazidi kuwa magumu katika mchakato wa uchaguzi mdogo wa mbunge Mbeya Vijijini baada ya kuzidi kwa matukio yanayopandisha joto zaidi la kisiasa mkoani Mbeya na hata maeneo mengine ya nchi.
Kuahirishwa kutangazwa kwa matokeo ya rufaa ya mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Sambwee Shitambala, hadi leo asubuhi, kumelimepandisha joto kwenye kinyang'anyiro cha kuziba nafasi iliyoachwa na mbunge wa CCM, Richard Nyaulawa.
Awali ilitaarifiwa kuwa uamuzi wa rufaa ya Shitambala, ambaye alienguliwa kugombea ubunge wa Mbeya Vijijini kwa kuapa kwa wakili badala ya hakimu, ingetolewa jana saa 4:00 asubuhi.
Lakini mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Lewis Makame aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa majibu ya rufaa yatatolewa leo saa 5:00 asubuhi wakati yale ya mgombea wa DP, Ndele Mboma yatatolewa saa 8:00 mchana.
Aliyasema hayo jana majira ya saa 10:00 jioni baada ya wagombea, walioenguliwa na msimamizi wa uchaguzi katika kinayang'anyiro cha ubunge katika Jimbo la Mbeya Vijijini na baadaye kukata rufaa, kuhojiwa na tume yake kwenye hoteli ya Mount Livingstone.
"Tumeshapitia rufaa za wagombea wote na majibu tutayatoa kesho saa 5:00 asubuhi kwa mgombea wa Chadema Sambwee Shitambala na saa 8:00 kwa mgombea wa DP, Ndele Mboma," alisema.
Aidha tume hiyo imeagiza wagombea hao wasiendelee na mikutano ya kampeni za uchaguzi, ikibatilisha uamuzi wa msimamizi wa uchaguzi wa Jimbo la Mbeya Vijijini, Juliana Malange, ambaye aliwaruhusu kufanya kampeni wakati wakisubiri majibu ya rufaa zao.
Mgombea wa Chadema alifanya mkutano wa kampeni juzi katika kata ya Utengule, Usongwe.
Akiongea baada ya kutoka kuhojiwa, Shitambala alisema kuwa alipata nafasi ya kutoa maelezo mengi kulingana na kosa lililosababisha aenguliwe katika uchaguzi huo, ikiwa ni pamoja na sheria inavyoelekeza katika masuala ya utoaji wa kiapo.
"Pia wametuhoji kuwa wamesikia kwamba tulifanya mkutano wa kampeni, tukamjibu ndiyo kwa kuwa msimamizi wa uchaguzi wa Jimbo la Mbeya Vijijini alituruhusu kuendelea na kampeni," alisema na kuongeza kuwa maamuzi hayo yalikuwa sahihi.
Shitambala alisema kuwa pamoja na maelezo hayo tume imewataka kutoendelea na kampeni hadi baada ya uamuzi kutangazwa kesho.
Habari kutoka ndani ya kikao hicho zinadai kuwa wajumbe wa tume hiyo, walianza mjadala wa rufaa hiyo mara baada ya kuwasili hotelini hapo saa 4:00 na kwamba, kulikuwa na mvutano mkubwa hadi majira ya saa 7:00 usiku wa kuamkia jana.
Inadaiwa kikao hicho kiliendelea tena jana asubuhi hadi saa 9:00 wakati walipowaita wagombea na kuwahoji na kumaliza saa 10:00 jioni.

Tuesday, December 30, 2008

Chadema Out Of Competition!


Fighting for political powers in My home Constituency!


http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=8905
Date::12/29/2008
Chadema yaenguliwa uchaguzi Mbeya vijijini
Na Brandy Nelson na Peter Edson
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeenguliwa kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Mbeya Vijijini baada ya mgombea wake, Sabwee Shitambala kuondolewa katika orodha ya wagombea kutokana na Tume ya Uchaguzi kukubali pingamizi dhidi yake lililowekwa na vyama viwili.
Kwa mujibu wa barua iliyotolewa na kusainiwa na mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi jimboni hapo, Juliana Malange mgombea huyo wa Chadema hataruhusiwa kushiriki kwenye uchaguzi huo ulioandaliwa kuziba pengo lililoachwa na Mbunge Richard Nyaulawa aliyefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.
"Kutokana na pingamizi lililowekwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF) maombi yao yamezingatiwa na hivyo mgombea wa Chadema hataweza kuendelea na kampeni zozote za uchaguzi," inaeleza sehemu ya barua hiyo.
Uongozi wa Chadema mkoani Mbeya ulithibitisha kupokea barua yenye maamuzi hayo na kusema kuwa wanatarajia kukaa kikao baadaye jana usiku ili kujua hatima ya chama chao.
Mamia ya mashabiki wa Chadema waliokuwa wamejikusanya katika ofisi za msimamizi wa uchaguzi walionekana kujikusanya katika makundi baada ya uamuzi huo kutolewa, wengi wakiilaani hatua hiyo ya tume ya uchaguzi.
Katibu mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa alisema amesikitishwa na uamuzi huo kwa kuwa umekifanya chama hicho pamoja na wadau wengine kupoteza imani na usimamizi unaoendelea katika mchakato wa kumpata mbunge atakayerithi kiti cha Marehemu Nyaulawa.
Alisema tayari wameshapata taarifa za pingamizi dhidi ya mgombea wao kwamba limetupiliwa mbali na lile la CUF na CCM kukubalika jambo ambalo alisema limezua utata ndani ya chama chake.
"Tunajiandaa kukata rufaa ndani ya masaa 48 yajayo ili tuweze kupata haki yetu ya msingi dhidi ya mgombea wetu ambaye tunaamini kuwa alikuwa na vigezo vyote vtya kushiriki kwenye uchaguzi," alisema Dk. Slaa.
"Mimi sipo Mbeya ila tumepewa taarifa kuwa ombi letu limetupiliwa mbali, wenzetu wa CCM na CUF wamekubaliwa... jambo hili limetufanya tupoteze imani," aliongeza.
Taarifa dhidi ya pingamizi ya mgombea wa chama hicho ziliwakilishwa kwa msimamizi huyo wa uchaguzi jimboni hapo zikieleza kuwa Shitambala alikwenda kuapa katika kampuni ya uwakili badala ya mahakama ya wilaya, kitendo ambacho kimeelezwa kuwa ni kinyume cha sheria.
Juzi Shitambala aliwekewa pingamizi na vyama vya CUF na CCM. Chadema ilimwekea pingamizi mgombea wa CCM kwa madai kuwa alisema uongo kuhusu mahali alipozaliwa.
Vuta nikuvute hiyo ilitokea katika ofisi ya msimamizi wa uchaguzi huo ambako CUF na CCM walidai kuwa mgombea wa Chadema aliapa kinyume na taratibu za uchaguzi.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwasilisha fomu ya pingamizi hilo, mjumbe wa tume ya uchaguzi ya CUF, Hussein Mmasi alisema chama chake kiliamua kumwekea pingamizi Shitambala kutokana na kuapa katika kampuni ya uwakili badala ya Mahakama ya Wilaya.
Madai hayo ndio pia yaliyoifanya CCM kumwekea pingamizi mgombea huyo.
Wakati huohuo, CUF imesema kuwa kinazitambua mbinu zinazotumiwa na CCM katika kuhakikisha kinapata ushindi kwa kuvuruga daftari la wapiga kura na kuongeza idadi watu kwa miujiza, ikidai kuwa hiyo ndiyo silaha yao kubwa.
Akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kuzindua kampeni uchaguzi wa ubunge Mbeya Vijijini, naibu katibu mkuu wa CUF, Duni Haji alisema kuwa chama chao kinahitaji mabadiliko na kimekuwa na nafasi kubwa ya kushinda katika chaguzi mbalimbali, lakini tatizo kubwa ni mbinu chafu zinazotumiwa na CCM.
Duni alisema kuwa CCM huvuruga daftari na kuongeza idadi ya wapiga kura kimiujiza na mwisho wake huwa ni matokeo ya kura kuonyeha idadi kubwa tofauti na idadi ya waliojiandikisha.
Naibu katibu huyo alifafanua kuwa mbinu nyingine ni ile ya kumwaga polisi vijijini ili kuwajengea hofu wananchi.
"Mbinu zote hizo zinazotumiwa na CCM zina lengo la kuwaibia kura wapinzani huku wakijua mshindi anapotangazwa, wapinzani huenda mahakamani, lakini hurudi mikono mitupu kwa kuwa wao ndio serikali," alisema.
Alisema kuwa pamoja na CCM kutumia mbinu hizo chafu, bado CUF haitakata tama kudai haki na kuendelea kuwaelimisha wananchi juu ya kuacha tabia ya kuuza shahada zao.

I can See Some You Now!

It is long time since I once saw some of you,I can now see you and some of you don't even know how I can see you.This is what we call Technology,It can just take seconds for me to get to see you pictures!
I can see those faces,I really miss you all an I wish you all A happy New Year!
But I don't know that very small kid!Everything has changed,Soon I will go to see all those changes.























































Monday, December 29, 2008

My Grandfather Is Growing Older!




















My lovely grandfather is growing Old and as he grows Old the house also grow old.I can see how lonely the grandparents are after all the other family members are away to other cities and countries.
I really thank you grandfather cause without you I don't know how I could have been today.I know you made me stronger and you fought for me in whatever Situation and may God bless you and give you a longer life.I will try to pay you back by doing something to the family and all those in need of my Help.I know there is nothing to pay back to you but just say thank you!
I will see you soon!
His name is Samwel A.Swila,He is one of the wonderful grandfather i have seen,He was ready to fight for me at whatever cost.Even if fighting for me was at the expense of his happiness he always fought.Whoever has lived with me It is all his work with the Help of his almighty.

Mchakato Wa Uchaguzu Mbeya Vijijini


Chadema Vs CCM in my Home!

http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=8873

Date::12/28/2008
Mgombea wa Chadema awekewa pingamizi
Brandy Nelson, Mbeya
MCHAKATO wa uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Mbeya Vijijini umeingia dosari baada ya mgombea wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)Sabwee Shitambala kuwekewa pingamizi na vyama vya CUF na CCM.
Wakati mgombea huyo wa Chadema akiwekewa pingamizi, Chadema imeeleza kumwekea pia pingamizi mgombea wa CCM kwa madai kuwa amesema uongo kuhusu mahala alipozaliwa.
Vuta nikuvute hiyo ilitokea jana katika ofisi ya msimamizi wa uchaguzi huo ambako CUF na CCM wamedai kuwa mgombea wa Chadema ameapa kinyume na taratibu za uchaguzi.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwasilisha fomu ya pingamizi hilo mjumbe wa tume ya uchaguzi ya CUF, Hussein Mmasi alisema chama chake kimeamua kumuwekea pingamizi mgombea wa Chadema kutokana na kuapa katika kampuni ya uwakili badala ya mahakama ya wilaya.
"Tumeweka pingamizi kutokana na mgombea wa Chadema kuapa katika kampuni ya uwakili ambako yeye anafanyia kazi. Kufanya hivyo ni sawa na mgombea huyo kujiapisha mwenyewe,"alisema.
Alisema taratibu za kisheria zinawataka wagombea kuapa mahakamani na siyo kwenye makampuni ya uwakili, kwani fomu ya mgombea wa Chadema inaonyesha mhuri wa kampuni ya mawakili ambayo ndiyo anayofanyia kazi.
Madai hayo ndio pia yaliyokifanya Chama Cha Mapindizi kumwekea pingamizi mgombea huyo.
Akizungumza na gazeti hili, Mkurugenzi wa vijana wa Chadema John Mnyika, alikiri kuwepo pingamizi hilo na kueleza kuwa chama kimejipanga kulipangua.
Alisema viapo vilikuwa wazi na Chadema imejipanga kuliondoa pingamizi hilo.
Akizungumzia suala la pingamizi la mgombea wake, Mnyika alisema limewekwa kimakosa kwani mawakili ambao ni makamishna wa uchaguzi wa wilaya wanaruhusiwa pia kuwaapisha wagombea.
Alisema mgombea wa Chadema alilazimika kuapishwa na wakili kutokana na mahakama kufungwa siku za sikukuu.
Katika hatua nyingine Chadema kimemwekea pingamizi mgombea wa CCM Mchungaji Luckson Mwanjali kwa madai kuwa mgombea huyo alitoa taarifa za uongo kuhusu mahali alipozaliwa.
Akizungumzia pingamizi hilo mjumbe wa kamati kuu ya Chadema na ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Mpanda Kati, Said Arfi alisema wameamua kutoa pingamizi hilo kutokana na mgombea huyo kutoa taarifa ya uongo kuwa ni mzaliwa wa Igawilo kitongoji cha Uyole jijini Mbeya huku taarifa zinaonyesha kuwa ni mzaliwa wa Tukuyu wilayani Rungwe.
"Tumeamua kuweka pingamizi dhidi ya mgombea wa CCM kutokana na kuwepo kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoa sababu za uongo za mahali alipozaliwa na tumemtaka mgombea huyo awasilishe vielelezo vitakavyothibitisha sehemu halali aliyozaliwa,"alisema.
Alizitaja sababu nyingine za pingamizi hilo kuwa ni Mgombea huyo kutotoa tamko
la kisheria kuhusu maslahi yake katika hospitali teule ya Wilaya ya Mbeya ya Ifisi
na kwamba siye mgombea aliyethibitishwa na chama chake cha CCM.